Kimataifa

West Ham Inamtaka Aaron Wan-Bissaka wa Man United

West Ham Inamtaka Aaron Wan-Bissaka wa Man United

Mazungumzo yanaendelea kati ya West Ham na Manchester United kuhusu uwezekano wa kumsajili beki wa kulia, Aaron Wan-Bissaka.

Klabu ya West Ham ina nia ya kujadili thamani ya mchezaji huyo ambayo inafahamika kuwa ni zaidi ya pauni milioni 15.

Wan-Bissaka ameingia mwaka wa mwisho wa mkataba wake na Manchester United na anataka kuangalia chaguo zake zote.

Mazungumzo kati ya Manchester United na Bayern Munich kuhusu beki wa kulia, Noussair Mazraoui, ambaye West Ham walikuwa na nia naye hapo awali, yanaelekea kuendelea vizuri.

Leave a Comment