Soka

Kikosi cha Yanga Vs Vitalo Leo, Agosti 24

Kikosi cha Yanga Vs Vitalo Leo

Kikosi cha Yanga Vs Vitalo Leo Agosti 24, 2024, Kikosi cha Yanga Leo Dhidi ya Vital’o Klabu Bingwa

Klabu ya Yanga SC leo itaikaribisha Vital’O katika mchezo wa marudiano wa michuano ya Klabu Bingwa Afrika CAF kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamanzi leo Agosti 24, majira ya saa moja usiku. Huu ni mchezo muhimu kwa Yanga, ambao walipata ushindi wa kishindo wa mabao 4-0 katika mechi ya awali dhidi ya mabingwa hao wa Burundi, Vital’O.

Katika mchezo wa leo, Yanga SC inahitaji kuhakikisha wanadumisha kasi yao na kupata matokeo mazuri ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa raundi inayofuata ya michuano hii ya kimataifa. Kocha wa Yanga, Miguel Gamondi, amesisitiza kwamba licha ya ushindi mzuri kwenye mechi ya awali, bado wana kazi kubwa ya kufanya kuhakikisha wanavuka salama hatua hii.

Kikosi cha Yanga Vs Vitalo Leo
Kikosi cha Yanga Vs Vitalo Leo

Kikosi Cha Yanga SC VS Vital’O Leo 24/08/2024

Hiki hapa ndicho kikosi rasmi cha Yanga leo

  • 59 Diarra
  • 21 Yad
  • 30 Kibabage
  • Mwamnyeto
  • 4 Bagga
  • Augho
  • Maxi
  • Mudathir
  • 24 Dube
  • 10 A212 Ki
  • 12 Chama

Yanga itaingia uwanjani ikiwa na kikosi chao kamili, ambacho kimejizatiti kutafuta ushindi mwingine mnono. Gamondi amethibitisha kuwa atashusha kikosi chenye nguvu, akilenga kuandikisha ushindi mkubwa zaidi.

Kikosi cha Yanga dhidi ya Vitalo Leo

Kikosi cha Yanga Leo dhidi ya Vitalo kinatarajiwa kutangazwa lisaa limoja kabla ya mchezo kuanza, hivyo endelea kutembelea ukurasa huu kupata taarifa kamili na orodha ya wachezaji wote watakao unda kikosi cha Yanga leo.

Tazama pia: Kikosi Cha Yanga SC VS Vital’O Leo: Wachezaji Wanaoanza

Mashabiki wa Yanga wanatarajiwa kufurika uwanjani leo, wakiwa na matumaini ya kuona timu yao ikipata ushindi mwingine mkubwa na kufuzu kwa raundi inayofuata ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika CAF. Kwa upande wa Vital’O, ingawa wanakabiliwa na kibarua kigumu, wana matumaini ya kupambana kwa uwezo wao wote na kuonyesha kwamba wao ni wapinzani wa kweli.

Kwa mashabiki wa soka, ni mechi inayotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa, ambapo Yanga SC inatazamia kuongeza nguvu na kuendelea kupeperusha bendera ya Tanzania kwenye michuano ya kimataifa.

Leave a Comment