Soka

Israel Mwenda Ailipua Singida Black Stars: “Makubaliano Yamevunjika

Israel Mwenda Ailipua Singida Black Stars

Israel Mwenda Afunguka Sakata Lake na Singida Black Stars

Baada ya taarifa zilizoripotiwa na MichezoLeo kuhusu Israel Mwenda, beki wa kulia aliyewahi kucheza Simba SC na sasa akisajiliwa na Singida Black Stars, mchezaji huyo ameibuka na madai mapya. Mwenda alikuwa amesaini mkataba mpya na Simba SC lakini aliamua kuomba kutafuta changamoto mpya nje ya klabu hiyo, na hivyo kuruhusiwa kuondoka. Nafasi yake Simba ilizibwa na Kelvin Kijiri aliyesajiliwa kutoka Singida Big Stars.

Israel Mwenda Alalamikia Kuvunjwa Kwa Makubaliano

Mwenda sasa anadai kuwa Singida Black Stars wamevunja makubaliano ya kimkataba, na amekuwa hana pa kwenda kwa sababu dirisha la usajili limefungwa. Ameeleza kuwa yupo kwenye mchakato wa kuvunja mkataba na anahisi kukosa mwelekeo katika mpira kutokana na hali hiyo.

Kauli ya Israel Mwenda Kuhusu Mkataba Wake

Israel Mwenda alisema:

“Nipo kwenye mchakato wa kuvunja mkataba, nyie subirini mtapata taarifa. Singida wapo nje ya makubaliano tuliyokubaliana. Mpira wetu una changamoto sana, halafu baadaye utasikia wazawa wana matatizo.”

Aliongeza kwa kusema:

“Nitaenda wapi sababu dirisha limefungwa? Hela niliyonayo inanitosha kuishi hata misimu minne bila kucheza mpira. Kiufupi ni kwamba sina timu.”

Changamoto za Wachezaji Wazawa Katika Soka

Mwenda amegusia changamoto zinazowakumba wachezaji wazawa katika soka la Tanzania, akibainisha kuwa wachezaji wengi wanakutana na matatizo ya kimkataba na kukosa nafasi za kucheza kutokana na masuala ya usajili na uvunjifu wa makubaliano na timu zao.

Kwa sasa, Mwenda anasubiri kupata suluhisho la mkataba wake na Singida Black Stars huku akionyesha kuwa na utayari wa kusubiri hadi usajili mwingine utakaporuhusiwa.


Mwenda ametoa onyo kali kuhusu hali ya mikataba kwa wachezaji wazawa, akionesha umuhimu wa timu kuheshimu makubaliano.

Leave a Comment