Soka

Historia ya Washindi wa Ngao ya Jamii Tanzania

Historia ya Washindi wa Ngao ya Jamii Tanzania

Ngao ya Jamii ni moja ya mashindano yanayovuta hisia nyingi katika soka la Tanzania, ikifungua msimu mpya wa ligi kwa mtanange mkali kati ya klabu bora za msimu uliopita. Mashindano haya yalianzishwa mwaka 2001 kwa lengo la kuleta mshikamano na furaha kwa mashabiki wa soka nchini.

Mwanzo wa Ngao ya Jamii

Ngao ya Jamii ilianza rasmi mwaka 2001 kwa mechi kali kati ya watani wa jadi, Simba na Yanga. Katika mchezo huo wa kihistoria, Yanga ilishinda kwa mabao 2-1, yaliyofungwa na Edibily Lunyamila na Ally Yussuph ‘Tigana’, huku bao pekee la Simba likifungwa na Steven Mapunda ‘Garincha’. Hata hivyo, mashindano haya hayakuendelea hadi mwaka 2009 yalipoanzishwa tena.

Orodha ya Washindi wa Ngao ya Jamii

Tangu kurejea mwaka 2009, Ngao ya Jamii imekuwa kipimo muhimu cha kuashiria mwanzo wa msimu mpya wa ligi kuu ya Tanzania. Hapa kuna orodha ya washindi wa Ngao ya Jamii miaka yote:

MwakaMshindiMatokeo
2001Yanga SC2-1 Simba SC
2009Mtibwa Sugar1-0 Yanga SC
2010Yanga SC3-1 Simba SC (Pen)
2011Simba SC2-0 Yanga SC
2012Simba SC3-2 Azam FC
2013Yanga SC1-0 Azam FC
2014Yanga SC3-0 Azam FC
2015Yanga SC8-7 Azam FC (Pen)
2016Azam FC4-1 Yanga SC (Pen)
2017Simba SC5-4 Yanga SC (Pen)
2018Simba SC2-1 Mtibwa Sugar
2019Simba SC4-2 Azam FC
2020Simba SC2-0 Namungo FC
2021Yanga SC1-0 Simba SC
2022Yanga SC2-1 Simba SC
2023Simba SC3-1 Yanga SC (Pen)
Washindi wa Ngao ya Jamii Miaka Yote
Washindi wa Ngao ya Jamii Miaka Yote

Mafanikio ya Simba na Yanga katika Ngao ya Jamii

Simba imefanikiwa kushinda Ngao ya Jamii mara kumi (10) tangu mwaka 2011 walipoifunga Yanga kwa mabao 2-0. Ushindi wao wa hivi karibuni ulikuwa mwaka 2023 dhidi ya Yanga kwa mikwaju ya penalti.

Kwa upande wa Yanga, wamechukua Ngao ya Jamii mara saba (7) tangu ushindi wao wa kwanza mwaka 2001. Ushindi wao wa hivi karibuni ulikuwa mwaka 2022 walipowashinda Simba kwa mabao 2-1.

Ushindani wa Ngao ya Jamii

Simba na Yanga ndizo klabu zinazotawala mashindano haya, zikileta burudani na ushindani mkubwa kwa mashabiki. Azam FC na Mtibwa Sugar pia zimeweza kujipatia ushindi kila moja mara moja, zikionyesha kuwa zina uwezo wa kushindana na vigogo wa soka nchini.

Leave a Comment