Soka

Matokeo ya Rayon Sports vs Azam FC – Mechi ya Kirafiki Agosti 3, 2024

Matokeo ya Rayon Sports vs Azam FC - Mechi ya Kirafiki Agosti 3, 2024

Matokeo ya Azam FC Dhidi Rayon Sports Mechi ya Kirafiki

Klabu ya Azam FC itachuana na wenyeji wao Rayon Sports katika mchezo wa kirafiki leo Agosti 3, 2024, saa 1:00 usiku katika Uwanja wa Amahoro. Mechi hii ni sehemu muhimu ya sherehe za mwaka za Rayon Sports Day, ambapo klabu hiyo itazindua rasmi jezi mpya, washirika wapya wa klabu, na kikosi kipya kitakachoshuka dimbani msimu wa 2024/25.

Matokeo ya Rayon Sports Vs Azam FC Leo Agosti 03 2024

Rayon SportsVSAzam Fc
  • Rayon Sports VS Azam FC
  • Mechi ya Kirafiki
  • Rayon Sports Vs Azam FC πŸ“† 03.08.2024
  • Uwanja wa Amahoro πŸ•– 7:00PM

Mchezo huu ni sehemu ya maadhimisho ya β€˜Rayon Sports Day’, ambapo klabu inawatambulisha wachezaji wapya, wadhamini wapya, na jezi mpya za msimu mpya. Sherehe hii ya mwaka huu itaambatana na β€˜Wiki ya Rayon’, ambapo klabu itafanya ziara nchini kote na kucheza michezo ya kirafiki katika miji ya Huye, Musanze, Rubavu na sehemu nyingine za Rwanda. Hii itakuwa mara ya saba kwa Rayon Sports kusherehekea siku hii maalum, ikiwa ni sehemu ya utamaduni wa klabu.

Mechi ya Rayon Sports Vs Azam FC inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na maandalizi makali ya timu zote mbili. Kwa Azam FC, mchezo huu utasaidia kutambua ubora wa kikosi na kujiweka sawa kwa mashindano makubwa yanayokuja. Kwa Rayon Sports, ni nafasi ya kuonesha uwezo wa wachezaji wapya na kuwaridhisha mashabiki wao kabla ya kuanza kwa msimu mpya.

Mashabiki wa soka wanatarajiwa kujitokeza kwa wingi kuunga mkono timu zao na kufurahia burudani ya soka la hali ya juu. Tunawatakia kila la heri timu zote mbili katika mchezo huu wa kirafiki na maandalizi yao ya msimu wa 2024/25.

Matokeo ya Rayon Sports vs Azam FC - Mechi ya Kirafiki Agosti 3, 2024
Matokeo ya Rayon Sports vs Azam FC – Mechi ya Kirafiki Agosti 3, 2024

Azam FC na Maandalizi kwa Ligi ya Mabingwa CAF

Azam FC inajiandaa kwa raundi ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika ya CAF msimu wa 2024/25, ambapo itakutana na APR FC. Mchezo huu wa kirafiki dhidi ya Rayon Sports utakuwa mtihani mzuri kwa mabingwa wa Rwanda na utawasaidia wachezaji wa Azam FC kuzoea hali ya hewa ya Kigali. Hii itakuwa fursa kwa kocha wa Azam FC kuwajaribu wachezaji wapya na kuimarisha muunganiko wa kikosi kabla ya kuanza kwa mashindano ya kimataifa.

Wachezaji Wapya na Matumaini Mapya kwa Rayon Sports

Rayon Sports inatarajia kutumia mchezo huu kujaribu wachezaji wapya waliowasajili kwa ajili ya msimu mpya. Wachezaji wapya walioungana na klabu ni pamoja na James Akaminko kutoka Ghana, aliyekuwa akichezea Azam FC, Patient Ndikuriyo, Fitina Omborenga, Richard Ndayishimiye, Omar Gning, Olivier β€˜Seif’ Niyonzima, Fiston Ishimwe, Emmanuel Nshimiyimana, Abdul Rahman Rukundo, Haruna Niyonzima, Prinsse Elenga-Kanga, na Adama Bagayogo. Bagayogo alifunga bao la kusawazisha katika sare ya 1-1 dhidi ya Gorilla FC kwenye Uwanja wa Kigali Pele siku ya Jumamosi.

Leave a Comment