Yanga SC

Prince Dube Afurahia Kucheza na Chama na Aziz Ki

Prince Dube Afurahia Kucheza na Chama na Aziz Ki

Mshambuliaji wa Yanga SC, Prince Dube, ameonyesha furaha yake ya kucheza pamoja na wachezaji wenye uwezo kama Clatous Chama na Aziz Ki, akisema kwamba uzoefu wao unamfanya kujituma zaidi na kuongeza hali ya kujiamini.

Dube, ambaye ni usajili mpya wa Yanga katika eneo la ushambuliaji, alitambulishwa rasmi Julai 7, kama zawadi maalum kwa mashabiki wa timu hiyo. Katika mchezo wa Toyota Cup dhidi ya Kaizer Chiefs nchini Afrika Kusini, ikiwa ni maandalizi ya msimu wa 2024/25, Dube alifunga bao la ufunguzi na kusaidia timu yake kushinda kwa mabao 4-0.

Baada ya ushindi huo, Yanga ilirejea Dar es Salaam kwa maandalizi ya Wiki ya Mwananchi, ambapo kilele cha tamasha hilo kinatarajiwa kuwa Agosti 4, Yanga itakapocheza dhidi ya Red Arrows.

Dube alisema: “Kucheza na wachezaji kama Chama na Aziz ni furaha kwangu. Wana uwezo mkubwa na wanachochea juhudi za timu kufanya vizuri zaidi.”

Leave a Comment