Yanga SC

Ali Kamwe Atinga na Manara Makao Makuu Baada ya Kujiuzulu

Ali Kamwe kaja na Manara Makao Makuu Baada ya Kujiuzulu

Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ali Kamwe, amewasiliana na waandishi wa habari Makao Makuu ya klabu hiyo siku moja tu baada ya kutangaza kujiuzulu kwake. Aliwahimiza mashabiki wa Yanga kwenda kukipokea kikosi chao kinachowasili leo.

Kamwe alifika na Haji Manara, lakini hajazungumza lolote kuhusu uamuzi wake wa kujiuzulu. Hata hivyo, taarifa za mitandaoni zimedai kwamba Rais wa Yanga, Hersi Said, na Makamu wake, Arafat Haji, walimzuia Kamwe kufanya maamuzi hayo, jambo ambalo linaaminika na wengi kuwa lilisababishwa na ujio wa Haji Manara.

Leave a Comment