Simba SC

Steven Mukwala na Shinikizo Kubwa Simba: Je, Ataweza Kuhimili?

Steven Mukwala na Shinikizo Kubwa Simba

Usajili wa mshambuliaji hatari kutoka Uganda, Steven Mukwala, umefanyika kwa mbwembwe kubwa chini ya uongozi wa Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally. Mukwala, ambaye aling’ara katika Ligi Kuu ya Ghana msimu uliopita kwa kuifungia Asante Kotoko mabao 14 katika mechi 28 na kutoa pasi mbili za mwisho, sasa anatarajiwa kuwa tishio kubwa katika safu ya ushambuliaji ya Simba.

Steven Mukwala na Shinikizo Kubwa Simba

Ahmed Ally alihakikisha mashabiki wa Simba wana imani kubwa na usajili huu, akisisitiza uwezo wa Mukwala katika kufumania nyavu, hasa kupitia mipira ya juu kutokana na umbile lake kubwa. Ahmed alifanya kazi ya kuwahakikishia mashabiki kuwa msimu huu Simba haitakuwa na matatizo katika safu ya ushambuliaji kama ilivyokuwa misimu iliyopita.

Hata hivyo, matarajio makubwa yaliyojengwa juu ya Mukwala yanaweza kumweka katika shinikizo kubwa. Mashabiki wengi wameamini kuwa yeye ndiye atakayekuwa mkombozi wa Simba baada ya miaka mitatu ya ukame wa mshambuliaji asilia. Kwa hiyo, Mukwala anahitaji kuwa makini katika kukabiliana na shinikizo hili, kwani bila mabao, itakuwa vigumu kumtetea mbele ya mashabiki wa Simba.

Mukwala anaonekana kuwa na kibarua kigumu zaidi katika kikosi cha Simba, hasa kutokana na sifa alizopata na nafasi anayocheza. Kwa mshambuliaji, mafanikio hupimwa kwa mabao, na mashabiki wa Simba tayari wameaminishwa kuwa Mukwala atatimiza matarajio hayo.

Leave a Comment