Simba SC

Sharti Gumu kwa Kibu Denis na Timu ya Norway

Sharti Gumu kwa Kibu Denis na Timu ya Norway

Klabu ya Simba sasa imeweka sharti gumu kwa mshambuliaji wake Kibu Denis na klabu ya Kristiansund BK inayomuhitaji. Ili Kibu kujiunga na timu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya Norway, Kristiansund BK inatakiwa kulipa Dola 1 milioni (Sh 2.7 bilioni). Vinginevyo, Simba haitakuwa tayari kumuachia mshambuliaji huyo kwa dau la chini.

Makosa Mawili Ya Kibu Denis Na Timu Yake Mpya

Mmoja wa viongozi wa Simba ameeleza kuwa uamuzi huo umechukuliwa ili kutoa fundisho kwa wachezaji na klabu za soka kuheshimu mikataba, kama inavyotakiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA). Alieleza makosa matatu makubwa yaliyofanyika katika suala la Kibu Denis. Kosa la kwanza ni mchezaji kuidanganya klabu na kutoroka akijua ana mkataba wa muda mrefu aliotoka kuusaini.

Kosa la pili ni timu ya Norway kufanya mazungumzo kinyume na kanuni za FIFA na mchezaji wa timu nyingine ambaye bado ana mkataba. Kosa la tatu ni Kibu kuharibu taswira ya klabu kwa kusema uongo kuhusu kutokuwepo kambini.

Kiongozi huyo alieleza kuwa Simba imetoa sharti kwa Kristiansund BK kulipa Dola 1 milioni ili kumvunja mkataba Kibu, na ikiwa hawatakubaliana, Simba itaishtaki klabu hiyo. Aliongeza kuwa klabu imesikia maombi kutoka upande wa mchezaji wa kutaka kuuza Kibu kwa dau wanalotaka wao, lakini Simba inasisitiza kuwa Kibu anunuliwe moja kwa moja kwa Dola 1 milioni badala ya kufanya majaribio ya mwezi mzima.

Kiongozi huyo aliongeza kuwa klabu ina ushahidi wa barua ya kuomba radhi kutoka Kristiansund BK na ofa waliyoiwasilisha mezani, pamoja na uthibitisho kutoka kwa Kibu mwenyewe.

Meneja wa Kibu Denis, Carlos Sylivester, alisema kuwa watajadili na Simba ili kupata suluhisho la tatizo hilo. Sylivester alisema kuwa Kibu anapaswa kufahamu kuwa hawezi kuikwepa Simba kwa kuwa ana mkataba nao, na ni vyema akae na viongozi wa Simba ili kumaliza suala hilo.

Simba imeweka wazi msimamo wake, na sasa inasubiri hatua za Kristiansund BK katika uhamisho wa Kibu Denis.

Leave a Comment