Yanga SC

Kikosi Cha Yanga Vs Azam Fc Fainali Ngao ya Jamii 11/08/2024

Kikosi Cha Yanga Vs Azam Fc Fainali

Kikosi Cha Yanga Vs Azam Fc Fainali Ngao ya Jamii 11/08/2024 | Kikosi cha Yanga Dhidi ya Azam Fc Fainali

Mtanange wa kukata na shoka unatarajiwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, Agosti 11, 2024, wakati Yanga na Azam FC zitakapokabiliana katika fainali ya Ngao ya Jamii msimu wa 2024. Mechi hii inakuja baada ya Azam FC kujikatia tiketi kwa ushindi mnono wa 5-2 dhidi ya Coastal Union, huku Yanga wakionyesha ubabe wao kwa kuwatoa mahasimu wao Simba kwa 1-0.

Fainali hii itakuwa ni mkutano wa 38 kati ya timu hizi mbili katika mashindano yote, ikiwa ni pamoja na Ligi Kuu Tanzania Bara, Kombe la Shirikisho la CRDB, na Kombe la Kagame la Cecafa. Yanga wanaongoza kwa ushindi katika mechi 17, huku Azam FC wakiwa wameshinda 10, na mechi 10 zikiisha kwa sare. Hata hivyo, historia haitakuwa na maana sana uwanjani Jumapili hii. Azam FC, wakiongozwa na kocha wao Bruno Ferry, wanatafuta kisasi baada ya kupoteza fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB kwa Yanga msimu uliopita.

Kikosi Cha Yanga Vs Azam Fc Fainali Ngao ya Jamii 2024

STARTING XI

  • 39 DIARRA
  • 21 YAO
  • 23 BOKA
  • 5 D.JOBC
  • 4 BACCA
  • 8 AUCHO
  • 7 MAXI
  • 38 ABUYA
  • 29 DUBE
  • 10 AZIZ KI
  • 26 PACOME

SUBSTITUTES

Khomeini, Kibabage, Mwamnyeto, Mkude, Mudathir, Chama, Musonda, Mzize, Baleke

Kikosi cha Yanga dhidi ya Azam FC kwa Fainali ya Ngao ya Jamii 2024 kinatarajiwa kuwa gumzo kubwa kwa mashabiki wa soka. Timu zote mbili zimejiandaa kwa mechi hii ya kihistoria, na wapenzi wa soka wanatazamia kuona majina ya nyota watakaopewa nafasi ya kuanza. Hata hivyo, vikosi rasmi vya timu hizi vitatangazwa rasmi saa moja kabla ya kipenga cha kuanza mchezo kupulizwa.

Leave a Comment