Simba SC

Kagoma Kukosa Dabi ya Kariakoo, Simba vs Yanga

Kagoma Kukosa Dabi ya Kariakoo, Simba vs Yanga

Simba yatangaza kuwa Kagoma atakosa Dabi ya Kariakoo dhidi ya Yanga kutokana na majeraha, akiweka shinikizo kwenye timu kabla ya msimu mpya.

Katika habari za hivi punde, kiungo mkabaji wa Simba, Yusuph Kagoma (28), atakaa nje ya uwanja kwa wiki mbili hadi tatu baada ya kupata majeraha akiwa kambini Ismailia, Misri.

Kagoma, ambaye alijiunga na Simba kutoka Singida Fountain Gate katika dirisha kubwa la usajili msimu uliopita, sasa atakosa mchezo muhimu wa Kariakoo Dabi unaotarajiwa kupigwa Agosti 8 mwaka huu kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.

Simba na Yanga zinatarajiwa kukutana katika nusu fainali ya Kombe la Ngao ya Jamii. Mara ya mwisho timu hizi zilipokutana, Simba ilipoteza kwa mabao 2-1, huku katika mzunguko wa kwanza wa msimu wa 2023/24 Simba ilichapwa 1-5.

Taarifa rasmi kuhusu majeraha ya Kagoma bado hazijatolewa, lakini kutokuwepo kwake kunaongeza changamoto kwa Simba katika maandalizi yao ya msimu mpya.

Leave a Comment