Simba SC

Jezi Namba 9 ya Simba: Jezi ya Gundu?

Jezi Namba 9 ya Simba

Jezi namba 9 ya Simba inahusishwa na gundu. Je, straika mpya Steven Mukwala ataweza kubadilisha imani hiyo?

Katika utambulisho mpya wa Simba, mshambuliaji Steven Mukwala amejitokeza akiwa na jezi namba 9, ambayo imekuwa na historia ya kuonekana kuwa na gundu ndani ya kikosi cha Simba.

Jezi hii mara ya mwisho ilivaliwa na mshambuliaji Laudit Mavugo kutoka Burundi, ambaye hakuweza kufanya vizuri na hatimaye akaachwa na timu.

Mshambuliaji mpya Steven Mukwala kutoka Asante Kotoko S.C ya Ghana, atakuwa na kazi ya kubadili dhana hii au ataikataa jezi hiyo kama wengine walivyofanya?

Wachezaji Waliovaa Jezi Namba 9

Zamoyoni Mogella – Simba Zamoyoni Mogella, mmoja wa washambuliaji hatari zaidi nchini, alicheza Simba kwa mafanikio makubwa akivaa jezi namba 9. Aliweza kufunga mabao mengi na hakuwa na hofu juu ya jezi hiyo.

Edward Chumila – Simba Edward Chumila aliingia Simba kuziba nafasi ya Mogella baada ya straika huyo kupata nafasi ya kwenda Uarabuni. Alivaa jezi namba 9 na kuwa kipenzi cha mashabiki wa Simba kwa kuwafunga mara kwa mara watani wao Yanga.

Wilker da Silva – Simba Mwaka 2019, Wilker da Silva, aliyesajiliwa kutoka Brazil, alichezea Simba kwa msimu mmoja tu akivaa jezi namba 9. Hata hivyo, hakuweza kufanya vizuri kutokana na majeraha ya mara kwa mara.

Betram Mwombeki – Simba Mwaka 2013, Betram Mwombeki alitua Simba kutoka Marekani na alianza na jezi namba 9 kabla ya kubadilisha na kuvaa namba 23.

Henry Joseph – Simba Baada ya kurejea kutoka Norway mwaka 2013, Henry Joseph alijiunga na Simba na alitakiwa kuvaa jezi namba 9. Hata hivyo, alikataa na kusema jezi hiyo haimvutii, na badala yake akachagua namba nyingine.

Gervas Kago – Simba Mwaka 2011, jezi namba 9 ilikuwa inavaliwa na Gervas Kago kutoka Jamhuri ya Kati, lakini hakufanya vizuri.

Blagnon na Mavugo – Simba Mwaka 2016, Laudit Mavugo kutoka Burundi aliomba jezi namba 9, lakini pamoja na Blagnon Frederick kutoka Ivory Coast, wote walishindwa kufanya vizuri.

Steven Mukwala ataweza kuvunja mikosi ya jezi namba 9 ndani ya Simba? Wakati utasema.

Leave a Comment