Soka

Ratiba Michezo ya Ngao ya Jamii 2024

Ngao ya Jamii

Michezo ya Ngao ya Jamii 2024 kuanza Agosti 8, Azam FC vs. Coastal Union na Yanga SC vs. Simba SC.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa ratiba rasmi ya mashindano ya Ngao ya Jamii kwa msimu wa 2024-25, yakianza Agosti 8 hadi Agosti 11, 2024. Hii ni ishara ya kuanza kwa msimu mpya wa soka nchini Tanzania, unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa na ubora wa juu.

Ratiba ya Ngao ya Jamii

TFF imetangaza ratiba kamili ya michezo na viwanja vitakavyotumika katika michuano ya Ngao ya Jamii ya mwaka huu. Msimu wa 2024/2025 utaanza Agosti 8 ambapo timu nne zitachuana kufikia fainali mnamo Agosti 11, 2024.

Ratiba ya Ngao ya Jamii
Ratiba ya Ngao ya Jamii

Ratiba Nusu Fainali Ngao ya Jamii 2024/2025

TareheMechiUwanja
8 Agosti 2024Azam FC vs. Coastal UnionUwanja wa Amaan, Zanzibar
8 Agosti 2024Young Africans vs. Simba SCUwanja wa Benjamin Mkapa, DSM

Agosti 8 itakuwa siku muhimu kwa mashabiki wa soka Tanzania. Azam FC itakutana na Coastal Union katika Uwanja wa Amaan, Zanzibar, huku Young Africans wakipambana na Simba SC katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Ratiba Fainali Ngao ya Jamii 2024/2025 na Mshindi wa Tatu

TareheMechiUwanja
11 Agosti 2024Mshindi wa TatuUwanja wa Benjamin Mkapa, DSM
11 Agosti 2024FainaliUwanja wa Benjamin Mkapa, DSM

Baada ya michezo ya nusu fainali, timu zitakazoshinda zitacheza fainali mnamo Agosti 11 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, ambapo bingwa mpya wa Ngao ya Jamii atatangazwa.

Timu Zinazoshiriki Ngao ya Jamii 2024/2025

Timu zinazoshiriki ni Yanga SC, Simba SC, Azam FC, na Coastal Union FC. Msimu uliopita, michezo ya Ngao ya Jamii ilifanyika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, na msimu huu, viwanja vya kisasa vinatarajiwa kutumika.

Michezo ya Ngao ya Jamii ni kipimo muhimu kwa timu kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu, ikiruhusu timu kujaribu vikosi na mbinu mpya huku mashabiki wakitarajia burudani kubwa.

Leave a Comment