HomeMichezoKikosi cha Simba VS Al Ahli Tripoli Tarehe 22 September 2024

Kikosi cha Simba VS Al Ahli Tripoli Tarehe 22 September 2024

Simba vs Al Ahli Tripoli: Kombe la Shirikisho CAF

Timu ya Simba Sports Club itakutana na Al Ahli Tripoli tarehe 22 Septemba 2024, katika mchezo wa kufuzu Kombe la Shirikisho la CAF. Mechi hii itapigwa majira ya saa 10:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki. Baada ya sare ya 0-0 katika mchezo wao wa kwanza, Simba inatarajia kuendeleza msururu wao wa kutofungwa na kupata matokeo bora mbele ya mashabiki wao.

Kikosi cha Simba VS Al Ahli Tripoli – Leo

Kuelekea mechi hii muhimu, Simba itategemea kikosi chake bora cha wachezaji. Hapa chini ni orodha ya kikosi cha Simba kinachotarajiwa kuanza dhidi ya Al Ahli Tripoli:

  1. Camara
  2. Kapombe
  3. Hussein
  4. Hamza
  5. Che Malone
  6. Kagoma
  7. Balua
  8. Fernandes
  9. Ateba
  10. Ahoua
  11. Mutale

Historia ya Mechi za Hivi Karibuni

Simba SC, maarufu kwa jina la “Wekundu wa Msimbazi,” wameonyesha uimara mkubwa katika mechi zao za hivi karibuni, hasa kwenye safu ya ulinzi. Timu hiyo imecheza mechi tano bila kufungwa, huku ikimaliza kila moja bila kuruhusu bao. Katika mechi ya kwanza dhidi ya Al Ahli Tripoli, Simba walifanikiwa kutoka na sare muhimu ugenini, jambo ambalo limeongeza matumaini ya kuibuka na ushindi nyumbani.

Soma: Matokeo Simba vs Al Ahli Tripoli – Leo Septemba 22, 2024

Kwa upande mwingine, Al Ahli Tripoli wana rekodi ya kutofungwa katika mechi nne mfululizo, na wanaingia katika mechi hii wakiwa na morali ya juu baada ya sare ya ugenini. Watahitaji kupata matokeo chanya ili kusonga mbele kwenye mashindano haya ya kimataifa.

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Latest Posts