Kikosi Rasmi Simba SC Kitakachoikabili Stellenbosch Nusu Fainali ya Pili CAF Confederation Cup
Klabu ya Simba SC imetangaza rasmi kikosi cha wachezaji 23 watakaosafiri kuelekea Afrika Kusini kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa Nusu Fainali ya Pili ya Kombe la Shirikisho la CAF (CAF Confederation Cup) msimu wa 2024/2025 dhidi ya Stellenbosch FC. Safari hiyo inatarajiwa kuanza Jumatano tarehe 23 Aprili 2025, asubuhi kupitia Shirika la Ndege la Air Tanzania kutoka Dar es Salaam hadi Johannesburg, kisha kuelekea mji wa Durban.
Mchezo huo muhimu utafanyika tarehe 27 Aprili 2025 kwenye Uwanja wa Moses Mabhida kuanzia saa 10:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki. Simba SC inakwenda kwenye mchezo huo ikiwa na faida ya ushindi wa bao 1-0 walioupata katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa kwenye uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Matokeo ya ushindi au sare ya aina yoyote katika mchezo huu wa marudiano yataihakikishia Simba kufuzu kwa mara ya kwanza kwenye Fainali ya CAF Confederation Cup.
Kikosi cha Simba SC Kitakachoikabili Stellenbosch Nusu Fainali ya Pili
Hiki hapa ni kikosi kamili cha wachezaji wa Simba SC watakaokabiliana na Stellenbosch:
Makipa
Na. | Jina |
---|---|
1 | Moussa Camara |
2 | Hussein Abel |
3 | Ally Salim |
Mabeki
Na. | Jina |
---|---|
4 | Chamou Karaboue |
5 | Mohamed Hussein |
6 | Shomari Kapombe |
7 | Abdurazack Hamza |
8 | David Kameta |
9 | Che Fondoh Malone |
10 | Valentino Nouma |
Viungo
Na. | Jina |
---|---|
11 | Joshua Mutale |
12 | Augustine Okejepha |
13 | Jean Charles Ahoua |
14 | Fabrice Ngoma |
15 | Awesu Awesu |
16 | Yusuph Kagoma |
17 | Kibu Denis |
18 | Debora Fernandes |
19 | Ladack Chasambi |
20 | Edwin Balua |
21 | Elie Mpanzu |
Washambuliaji
Na. | Jina |
---|---|
22 | Steven Mkwala |
23 | Leonel Ateba |
Simba SC sasa inaelekea kwenye moja ya mechi zake muhimu zaidi katika historia ya mashindano ya CAF, ikisaka tiketi ya kuandika historia mpya kwa kushiriki fainali ya michuano hiyo mikubwa barani Afrika.