Biashara

Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024

Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024

Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024, LATRA Yatangaza Nauli za SGR, Safari Kuanza Hivi Karibuni

Watanzania wanaosubiri kwa hamu uzinduzi wa safari za treni ya mwendokasi (Standard Gauge Railway – SGR) sasa wana sababu ya kutabasamu. Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imezindua rasmi nauli zitakazo tumika kwenye safari za treni ya mwendokasi kwa mwaka 2024, huku safari za abiria kutajwa kuanza hivi karibuni. Huu ni wakati wa kihistoria kwa sekta ya usafiri wa reli nchini, kwani SGR inatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa katika jinsi tunavyosafiri.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na LATRA, nauli za SGR zimewekwa kwa kuzingatia umbali wa safari na umri wa abiria, hivyo kuhakikisha kuwa usafiri huu wa kisasa unakuwa nafuu na haki kwa Watanzania wote. Kuanzia Dar es Salaam hadi Pugu, Morogoro, Dodoma, na hata mikoa ya mbali zaidi kama Makutupora, sasa unaweza kusafiri kwa treni ya kisasa, yenye kasi na urahisi usio na kifani.

Muundo wa Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024

Nauli za SGR zimewekwa kwa kuzingatia umbali wa safari usika na umri wa abiria. Kwa watu wazima na watoto wenye umri zaidi ya miaka 12, nauli imetajwa kuwa ni Tsh. 69.51 kwa kila kilomita. Watoto wenye umri kati ya miaka 4 na 12 watalipa nusu ya bei hiyo, yaani Tsh. 34.76 kwa kilomita. Watoto chini ya miaka minne watasafiri bure, lakini taarifa zao zitahitajika kurekodiwa.

Hizi ndizo Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024 Kwa Abiria Wenye umri zaidi ya miaka 12

Mchanganuo wa nauli hizo kwa daraja la kawaida kulingana na umbali wa vituo kuanzia Dar es Salaam hadi Makutupora kwa watu wazima na watoto wenye umri zaidi ya miaka 12 ni kama ifuatavyo;

Safari Umbali (Km)Nauli (Shilingi)
KutokaKwendaDaraja la Kawaida
Dar es SalaamPugu191000
Dar es SalaamSoga514000
Dar es SalaamRuvu735000
Dar es SalaamNgerengere134.59000
Dar es SalaamMorogoro19213000
Dar es SalaamMkata22916000
Dar es SalaamKilosa26518000
Dar es SalaamKidete31222000
Dar es SalaamGulwe354.725000
Dar es SalaamIgandu387.527000
Dar es SalaamDodoma44431000
Dar es SalaamBahi501.635000
Dar es SalaamMakutupora53137000

Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024 Kwa Abiria Wenye umri Kuanzaia Miaka 4 hadi 12

Aidha, mchanganuo wa nauli kwa daraja la kawaida kulingana na umbali wa vituo kuanzia Dar es Salaam hadi Makutupora kwa watoto wenye umri kuanzia miaka minne (4) hadi 12 ni kama ifuatavyo;

SafariUmbali (Km)Nauli (Shilingi)
KutokaKwendaDaraja la Kawaida
Dar es SalaamPugu19500
Dar es SalaamSoga512000
Dar es SalaamRuvu732500
Dar es SalaamNgerengere134.54500
Dar es SalaamMorogoro1926500
Dar es SalaamMkata2298000
Dar es SalaamKilosa2659000
Dar es SalaamKidete31211000
Dar es SalaamGulwe354.712500
Dar es SalaamIgandu387.513500
Dar es SalaamDodoma44415500
Dar es SalaamBahi501.617500
Dar es SalaamMakutupora53118500
Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024
Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024

Masharti Kabla ya Safari Kuanza

LATRA imetoa masharti kadhaa ambayo yanapaswa kutimizwa kabla ya kuanza kwa safari za SGR. Masharti haya ni pamoja na:

  • Shirika la Reli Tanzania (TRC) kuwa na leseni ya usafirishaji
  • Miundombinu ya reli na mabehewa kuwa na ithibati ya usalama
  • Matumizi ya mfumo wa utoaji tiketi za kielektroniki
  • Kuunganishwa kwa mfumo wa tiketi na mifumo ya LATRA
  • Uwepo wa watumishi waliothibitishwa na waliosajiliwa na LATRA

Leave a Comment