Ajira Tanzania

NAFASI za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa – Kagera

NAFASI za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa anakaribisha maombi ya ajira kufuatia kibali kilichotolewa kwa mwaka wa ikama 2023/2024. Watanzania wenye sifa na uwezo wanahimizwa kutuma maombi kwa nafasi ifuatayo:

Msaidizi wa Maendeleo ya Jamii Daraja la II – Nafasi 06

Majukumu ya Kazi

  • Kuratibu shughuli za maendeleo ya jamii kwa kuzingatia jinsia.
  • Kuhamasisha jamii kushiriki katika kupanga, kutekeleza, na kutathmini miradi yao ya maendeleo.
  • Kutoa elimu kuhusu masuala ya kijinsia na kuondoa mila potofu.
  • Kuelimisha jamii kuhusu teknolojia sahihi na matumizi yake.
  • Kukusanya na kuchambua takwimu za kijamii kwa ajili ya kupanga mipango bora.
  • Kuelimisha jamii kuhusu haki za watoto na umuhimu wa elimu ya watu wazima.
  • Kutoa taarifa za utekelezaji wa kazi kila mwezi.
  • Kufanya kazi nyingine kama atakavyoelekezwa na mkuu wake wa kazi.

Sifa za Mwombaji

  • Awe raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 18 hadi 45.
  • Awe na Cheti cha Kidato cha Nne (IV) au Sita (VI).
  • Awe amehitimu Astashahada/Cheti katika Maendeleo ya Jamii au Sayansi ya Sanaa kutoka taasisi inayotambuliwa na serikali.

Mshahara

Ngazi ya mshahara wa serikali – TGS B.

Masharti ya Jumla kwa Waombaji

  • Kuambatanisha cheti cha kuzaliwa kilichothibitishwa na mwanasheria.
  • Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na kuainisha ulemavu wao katika mfumo wa ajira.
  • Kuambatisha wasifu binafsi (CV) yenye maelezo kamili pamoja na majina ya wadhamini watatu.
  • Kuambatanisha nakala za vyeti vya taaluma vilivyothibitishwa na mwanasheria.
  • Waombaji waliomaliza masomo nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimeidhinishwa na mamlaka husika (NECTA, NACTE, TCU).
  • Waombaji waliostaafu utumishi wa umma hawaruhusiwi kuomba bila kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
  • Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 05 Aprili 2025, saa 6:00 usiku.

Jinsi ya Kutuma Maombi

Waombaji wote wanapaswa kutuma maombi yao kupitia mfumo wa Ajira Recruitment Portal kwa anuani ifuatayo:
🔗 https://portal.ajira.go.tz

DOWNLOAD PDF FILE HAPA

Maombi yote yaelekezwe kwa:
MKURUGENZI MTENDAJI,
HALMASHAURI YA WILAYA YA KYERWA,
S.L.P 72, KYERWA.

Maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu hayatazingatiwa.

Leave a Comment