Ajira Tanzania

NAFASI MPYA ZA AJIRA KAHAMA MUNICIPAL COUNCIL 2025

Ajira Mpya Kahama Municipal Council Mei 2025

Ajira Mpya Kahama Municipal Council Mei 2025

Halmashauri ya Manispaa ya Kahama imetangaza nafasi mpya za ajira kwa mwaka wa fedha 2024/2025, kufuatia kibali cha ajira kutoka Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilichotolewa tarehe 29 Aprili 2025. Watanzania wenye sifa wanakaribishwa kutuma maombi kuanzia Mei 14, 2025.

Nafasi Zinazotangazwa:

1. Msaidizi wa Kumbukumbu Daraja II – Nafasi 04

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya kidato cha nne au sita
  • Stashahada (NTA Level 6) katika:
    • Utunzaji wa Kumbukumbu
    • Urasimu Ramani (Cartography)
    • Geo-Informatics
    • Sheria
    • Kumbukumbu za Afya
  • Ujuzi wa matumizi ya kompyuta kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali

Majukumu:

  • Kuorodhesha barua zinazoingia na kutoka
  • Kusambaza na kupokea majalada
  • Kutafuta na kurudisha kumbukumbu
  • Kufuatilia mzunguko wa majalada

Mshahara: Kwa mujibu wa ngazi ya serikali ya TGS C1

2. Dereva Daraja II – Nafasi 03

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya kidato cha nne au sita (kuanzia daraja la nne)
  • Mafunzo ya msingi ya uendeshaji magari kutoka VETA, NIT au chuo kinachotambuliwa na serikali
  • Leseni ya daraja C au E
  • Awe mwadilifu na hajawahi kutiwa hatiani

Majukumu:

  • Kukagua usalama wa gari
  • Kuwasafirisha watumishi
  • Kusambaza nyaraka
  • Kuhifadhi taarifa za safari
  • Kufanya usafi wa gari

Mshahara: Kwa mujibu wa ngazi ya serikali ya TGS B1

Masharti ya Jumla kwa Waombaji Wote:

  • Awe Mtanzania mwenye umri kati ya miaka 18 hadi 45
  • Ambatanisha nakala ya cheti cha kuzaliwa
  • Ambatanisha C.V yenye taarifa binafsi na namba za simu
  • Ambatanisha vyeti vya elimu na taaluma vilivyothibitishwa na wakili au Kamishna wa viapo
  • Vyeti vya nje ya nchi lazima vifanyiwe ulinganishi na TCU au NACTE
  • Ambatanisha picha moja ya “passport size” ya hivi karibuni
  • Maombi yaandikwe kwa Kiswahili au Kiingereza na yasainiwe

Jinsi ya Kutuma Maombi:

Tuma maombi kupitia Mfumo wa Kielektroniki wa Ajira kwa anuani:
🔗 https://portal.ajira.go.tz

Anuani ya barua:
Mkurugenzi wa Manispaa,
Barabara ya Boma,
S.L.P 472,
KAHAMA – Shinyanga.

⚠️ Maombi yatakayowasilishwa nje ya mfumo huu hayatazingatiwa.


🗓 Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 27 Mei, 2025. Usikose fursa hii ya kujiunga na Manispaa ya Kahama.

Leave a Comment