Kikosi Rasmi cha Simba SC vs Stellenbosch 20/04/2025

0
Kikosi Rasmi cha Simba SC vs Stellenbosch 20/04/2025

Kikosi cha Simba SC Leo Dhidi ya Stellenbosch – CAFCC Nusu Fainali 20 April 2025

Simba SC inaingia uwanjani leo Jumapili, tarehe 20 Aprili 2025, kuivaa Stellenbosch FC ya Afrika Kusini katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC). Mechi hii muhimu inachezwa kwenye Uwanja wa Aman Complex, na kocha Fadlu Davids ametoa tahadhari kwa wachezaji wake dhidi ya kulewa sifa kabla ya kazi kukamilika.

Kocha Davids amesema kuwa kufuzu kwa hatua ya nusu fainali si mafanikio ya mwisho, bali ni hatua muhimu kuelekea malengo makubwa zaidi. Ametaka wachezaji waweke akili na nguvu zao zote kwenye mechi hii ya kwanza, kwani inatoa nafasi nzuri kwa Simba kupata matokeo chanya kabla ya mchezo wa marudiano nchini Afrika Kusini.

Katika taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Simba SC itaanzia nyumbani kabla ya kusafiri kwa mkondo wa pili wa nusu fainali. Hii ni nafasi adhimu kwa wawakilishi wa Tanzania kutinga hatua ya fainali kwa mara ya kwanza katika historia yao kwenye mashindano haya ya kimataifa.

Kikosi cha Simba SC Leo Dhidi ya Stellenbosch – 20/04/2025

NAMCHEZAJI
1Moussa Camara
2Shomari Kapombe
3Zimbwe Jr
4Hamza
5Chamou Karaboue
6Fabrice Ngoma
7Yusuf Kagoma
8Stephane Ahoua
9Elie Mpanzu
10Clatous Chama ‘Kibu’
11Steven Mukwala
Kikosi Rasmi cha Simba SC vs Stellenbosch 20/04/2025

Kikosi hiki kinaonyesha dhamira ya Simba SC kuanza kwa nguvu mbele ya mashabiki wake na kujiweka katika nafasi nzuri kuelekea mchezo wa marudiano wiki ijayo.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here