Jinsi Ya

Bei za Tiketi na Ratiba ya Treni ya Umeme SGR Dar es Salaam hadi Dodoma 2024

Bei za Tiketi na Ratiba ya Treni ya Umeme SGR Dar es Salaam hadi Dodoma 2024

Safari za Treni ya Umeme SGR Dar hadi Dodoma Zimeanza Rasmi

Treni ya umeme ya SGR kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma imeanza rasmi kutoa huduma, ikiwapa wasafiri nafasi ya kufurahia safari za haraka na za kisasa. Huduma hii mpya inajulikana kama “express train,” ikiwaleta wasafiri Dodoma kwa muda mfupi zaidi huku wakifurahia huduma za kipekee ndani ya treni.

Ratiba ya Safari na Vituo

Treni ya umeme ya SGR inaanza safari zake rasmi Julai 25, 2024. Treni inatoka Dar es Salaam saa 12:00 asubuhi na kufika Dodoma saa 3:25 usiku, ikichukua saa tatu na dakika 25 pekee. Treni itasimama Morogoro kabla ya kufika Dodoma. Kwa wasafiri wanaotumia treni ya kawaida, safari itaanza saa 3:30 asubuhi kutoka Dar es Salaam na kufika Dodoma baada ya kusimama kwenye vituo vidogo kama Pugu.

Nauli ya Treni ya Umeme ya SGR

Nauli zinatofautiana kulingana na aina ya treni na daraja la huduma:

Treni ya Kawaida:

  • Tsh 31,000 kwa safari ya kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma.

Treni ya Haraka (Express Train):

  • Daraja la Biashara: Tsh 70,000
  • Daraja la Juu: Tsh 120,000
Bei za Tiketi na Ratiba ya Treni ya Umeme SGR Dar es Salaam hadi Dodoma 2024
Bei za Tiketi na Ratiba ya Treni ya Umeme SGR Dar es Salaam hadi Dodoma 2024

Bei ya Tiketi Treni ya Mwendokasi SGR 2024 Kwa Abiria Wenye umri zaidi ya miaka 12

Bei ya Tiketi za Treni Ya Mwendokasi kwa daraja la kawaida kulingana na umbali wa vituo kuanzia Dar es Salaam hadi Makutupora kwa watu wazima na watoto wenye umri zaidi ya miaka 12 ni kama ifuatavyo;

Safari VituoUmbali (Km)Nauli (Shilingi)
KutokaKwendaDaraja la Kawaida
Dar es SalaamPugu191000
Dar es SalaamSoga514000
Dar es SalaamRuvu735000
Dar es SalaamNgerengere134.59000
Dar es SalaamMorogoro19213000
Dar es SalaamMkata22916000
Dar es SalaamKilosa26518000
Dar es SalaamKidete31222000
Dar es SalaamGulwe354.725000
Dar es SalaamIgandu387.527000
Dar es SalaamDodoma44431000
Dar es SalaamBahi501.635000
Dar es SalaamMakutupora53137000

Bei Ya Tiketi Kwa Abiria Wenye umri Kuanzaia Miaka 4 hadi 12

Aidha, mchanganuo wa Bei ya tiketi za Treni ya mwendokasi kwa daraja la kawaida kulingana na umbali wa vituo kuanzia Dar es Salaam hadi Makutupora kwa watoto wenye umri kuanzia miaka minne (4) hadi 12 ni kama ifuatavyo;

SafariVituoUmbali (Km)Nauli (Shilingi)
KutokaKwendaDaraja la Kawaida
Dar es SalaamPugu19500
Dar es SalaamSoga512000
Dar es SalaamRuvu732500
Dar es SalaamNgerengere134.54500
Dar es SalaamMorogoro1926500
Dar es SalaamMkata2298000
Dar es SalaamKilosa2659000
Dar es SalaamKidete31211000
Dar es SalaamGulwe354.712500
Dar es SalaamIgandu387.513500
Dar es SalaamDodoma44415500
Dar es SalaamBahi501.617500
Dar es SalaamMakutupora53118500

Upatikanaji wa Tiketi

Tiketi za treni zinapatikana kwa njia ya mtandao kupitia tovuti rasmi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC) na pia katika stesheni za SGR. Kwa muongozo wa jinsi ya kukata tiketi mtandaoni, tafadhali angalia chapisho letu, “Jinsi Ya kukata Tiketi Ya Treni Online.” Hii inawawezesha wasafiri kupanga safari kwa urahisi na kwa wakati wao, huku wakihakikisha wanapata tiketi mapema.

Leave a Comment