TAALUMA ZINAZOHITAJIKA KUJIUNGA NA JWTZ MWAKA 2025
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limetangaza nafasi maalum za uandikishaji kwa vijana wa Kitanzania wenye elimu ya Sekondari hadi Vyuo Vikuu, likilenga kuajiri wataalamu wa taaluma adimu zinazohitajika kwa maendeleo ya jeshi.
Uandikishaji huu maalum unalenga kutoa fursa kwa vijana wenye taaluma muhimu kujiunga na jeshi, ambapo wataendelea kupata mafunzo ya kijeshi pamoja na maendeleo katika taaluma zao binafsi. JWTZ inalenga kuimarisha ufanisi wake kwa kujumuisha wataalamu waliobobea katika sekta mbalimbali muhimu.
Taaluma za Tiba Zinazohitajika
JWTZ inahitaji wataalamu wa afya waliobobea katika maeneo yafuatayo:
Madaktari Bingwa
- General Surgeon
- Orthopaedic Surgeon
- Urologist
- Radiologist
- ENT Specialist
- Anaesthesiologist
- Physician
- Ophthalmologist
- Paediatrician
- Obstetrician Gynaecologist
- Oncologist
- Pathologist
- Psychiatrist
- Emergency Medicine Specialist
- Haematologist
Wataalamu wa Afya na Sayansi Shirikishi
- Medical Doctor
- Dental Doctor
- Veterinary Medicine
- Bio Medical Engineer
- Dental Laboratory Technician
- Anaesthetic
- Radiographer
- Optometry
- Physiotherapy
- Aviation Doctor
Taaluma za Uhandisi Zinazohitajika
JWTZ pia inahitaji wahandisi waliobobea katika fani mbalimbali zifuatazo:
- Bachelor of Electronic Engineering
- Bachelor of Mechanical Engineering
- Bachelor in Marine Engineering
- Bachelor in Marine Transportation and Nautical Science
- Bachelor in Mechanics in Marine Diesel Engine
- Bachelor in Aviation Management
- Bachelor in Aircraft Accident and Incident Investigation
- Bachelor in Meteorology
- Air Traffic Management
- Aeronautic Engineering
Jeshi la Ulinzi linaendelea kuimarisha safu yake ya wataalamu kupitia vijana wa Kitanzania waliobobea katika taaluma hizi, likiwa na dhamira ya kuhakikisha ulinzi wa taifa unakuwa wa kisasa na wa kitaalamu zaidi.